NEWS

AFYA

STORI ZA KITAA

Latest Release

Monday 19 March 2018

 Naibu Katibu Mkuu Wazazi ccm Tanzania bara
Godfrey Mheluka akiwa anawahutumia wananchi waliouthuria katika
kongamano la kujadili maadili mema   na uzalendo  ni ustawi wa Arusha
yetu na Taifa letu  kwa ujumla ,kongamano lililoandaliwa na Jumuiya ya
Wazazi ya Chama cha Mapinduzi (CCM)mkoa wa Arusha ,kongamano ambalo
lilishirikisha wananchi ,viongozi wa dini ,vyombo vya usalama pamoja
na viongozi mbalimbali wa serikali pamoja na wa sekta binafsi
iliyofanyikia katika ukumbi wa Triple A uliopo ndani ya jiji la Arusha
kamanda wa vijana  UVCCM mkoa wa Arusha  Philemon
Molel maarufu kama Monabani akiongea na wananchi waliouthuria katika
kongamano la kujadili maadili mema   na uzalendo  ni ustawi wa Arusha
yetu na Taifa letu  kwa ujumla ,kongamano lililoandaliwa na Jumuiya ya
Wazazi ya Chama cha Mapinduzi (CCM)mkoa wa Arusha ,kongamano ambalo
lilishirikisha wananchi ,viongozi wa dini ,vyombo vya usalama pamoja
na viongozi mbalimbali wa serikali pamoja na wa sekta binafsi
iliyofanyikia katika ukumbi wa Triple A uliopo ndani ya jiji la Arusha
Habari picha na  Woinde Shizza,Arusha
Wazazi wametakiwa kutimiza wajibu  wao wa kuwalea watoto  kwakufuata
maadili ya Mtanzania na kuacha kuiga tamaduni  za kigeni  ,kwani
baadhi ya tamaduni za kigeni wanazo ziiga zinachangia kusababisha
mporomoko wa maadili katika jamii zetu .
Hayo yamebainishwa na Naibu Katibu Mkuu Wazazi ccm Tanzania bara
Godfrey Mheluka wakati akifunga kongomano  la kujadili  maadili mema
na uzalendo  ni ustawi wa Arusha yetu na Taifa letu  kwa ujumla
,kongamano lililoandaliwa na Jumuiya ya Wazazi ya Chama cha Mapinduzi
(CCM)mkoa wa Arusha ,kongamano ambalo lilishirikisha wananchi
,viongozi wa dini ,vyombo vya usalama pamoja na viongozi mbalimbali wa
serikali pamoja na wa sekta binafsi iliyofanyikia katika ukumbi wa
Triple A uliopo ndani ya jiji la Arusha

Alisema kuwa  wazazi wengi wa wamekuwa wanalea watoto kwa kufuata
tamaduni za wenzetu wan chi za nje wakidai kuwa ndio malezi bora kwa
watoto na yakisasa kitu ambacho sio kizuri kwani baadhi ya tamaduni za
wenzetu ukiangalia za kutoka nchi za kimagharibi  zinaporomosho
maadili kwa watoto wetu.
“ukithamini tamaduni za kimagharibi na ukaacha za kwetu na ukamuacha
mtoto nae akathamini tamaduni hizohizo ujue umempoteza mtoto na
umemuaribu kabisa unakuta mzazi anaona mtoto anavaa mlegezo au kimini
badala ya kumkataza anamuacha anaona kuwa wake ndio mjanja huo sio
ujanja ni ujinga ni kumuaribu mtoto unatakiwa umwambie mtoto hivi sio
vyema ivi nikiwauliza wazazi ivi nyie mngelelewa hivyo  au mngelelewa
vibaya je leo mngekuwepo apo mlipo  ni wajibu wetu kuwalea watoto wetu
kwa kufuata utamaduni wetu mzuri wenye maadili ili kuweza kuandaa
viongozi wazuri wa baada na wazazi wazuri wa baadae “alisema Mhekuka

Kwa upande wake mwenyekiti wa jumuiya ya  wazazi ccm mkoa wa Arusha
Dr,John Palanjo alisema ni wazazi anatakiwa kutimiza waji wake kwa
mtoto wake huku pia mtoto akitakiwa kutimiza wajibu wake kwa mzazi
,aliongeza kuwa pia niwajibu wa kila mzazi kumfatilia mtotowake na
kujua maendeleo yake mwenyewe na sio kumuachia mwalimu amfatilie au
dada wa kazi amfatilie huku akibainisha kuwa mzazi yeyote asitafute
mchawi wa mtoto wake kwani ,asilimia kubwa ya wazazi wao wenyewe ndio
wachawi wawatoto wao.
Aidha aliwaasa wazazi kutenga mda wa kukaa na watoto wao na kuongea na
kuwaelezea kipi kibaya na kipi kizuri ili kuwawezesha watoto wetu
kukuwa  kwa kuendana  na yale   yanayopendeza kwa jamii inayowazunguka
.

“mimi na imaini iwapo mzazi akijua wajibu wake atakubali hata kidogo
mtoto wake aharibike ,hivyo ni vizuri mzazi utambue  wajibu  wako
umrudie mungu  usali maana ukiwa na hofu ya mungu lazima utamlea mtoto
kwa kufuata kanuni za kimungu”alisema katibu wa  wawazazi wilaya ya
Arusha Christoper Pallangyo

Kwa upande wake mwenyekiti wa wazazi wilaya  ya Arusha Ally Meku
aliwataka baadhi ya wazazi   kupunguza migogoro  ndani ya familia ili
watoto nao wasiige tabia mbaya kwani  wanapoaanza migogo katika
familia wanashindwa kuwale watoto wao na badala yake watoto hao
wanaanza kutangatanga hovyo na kuanza kuiga tabia mbaya.
 baadhi ya viongozi wakiwa wanaimba na kucheza

 baadhi ya viongozi wakiwa meza kuu wanafatilia kongamano
 RTO  wa mkoa wa Arusha Josephy Bukombe nae alikuwepo katika kongamano hilo ambapo aliwasisitiza wazazi na vijana waliouthuria katika kongamano hilo kufuata maadili ,huku akiwasihi wazazi  kuwakumbusha vijana wao kuvaa kofia ngumu wakati wanapoendesha pikipiki zao pamoja na kufuata sheria za usalama barabarani ili kupunguza ajali ambazo zinaweza kutokea mara kwa mara
 mkuu wa wilaya ya Arusha akiongea na wananchi waliouthuria katika kongamano hilo
 wanafunzi wa shule ya sekondari ya Edmond Rice nao waliuthuria katika kongamano hilo


  mwenyekiti wa jumuiya ya  wazazi ccm mkoa wa Arusha
Dr,John Palanjo akiongea na wananchi waliouthuria katika kongamano hilo

 Ofisa mradi wa Mbegu za Mahindi yanayostahimili  Ukame ya Wema 2109  kutoka Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) kupitia Jukwaa na Bioteknolojia kwa Maendeleo ya Kilimo (OFAB), Bestina Daniel, akizungumza wakati wa uzinduzi wa shamba darasa la mbegu hiyo katika Kijiji cha Kilemela kilichopo Kata ya Kerege wilayani Bagamoyo jana. W a pili kutoka kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Majid Mwanga na hao wengine ni viongozi mbalimbali katika wilaya hiyo.
 Ofisa Kilimo wa Mkoa wa Pwani, Kapilima George akizungumza.
 Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Majid Mwanga, akitoa hutuba yake.
 Mkurugenzi wa Fedha wa Fedha na Utawala wa COSTECH,Shabani Hussein (kulia), akimkabidhi Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Majid Mwanga  mbegu hizo kabla ya kuzindua shamba darasa. Katika ni Ofisa mradi wa Mbegu za Mahindi yanayostahimili  Ukame ya Wema 2109  kutoka Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) kupitia Jukwaa na Bioteknolojia kwa Maendeleo ya Kilimo (OFAB), Bestina Daniel.
 Mwakilishi wa Kikundi cha Kikuki Malengo Group kutoka Kitongoji cha Amani, Othman Said Ally akikabidhiwa mbegu. Wa pili kulia ni Mtafiti  Kutoka Kituo cha Utafiti wa Kilimo cha Ilonga mkoani Morogoro, Nikidadi Hamidu.
 Mkulima Julius Maina (kushoto), kutoka Kitongoji cha Zinga akikabidhiwa mbegu.
 Mkulima Anaseli Macha kutoka Kijiji cha Kongo Kaya ya Yombo akikabidhiwa mbegu.
 Mkulima Ahazi Mwasibata akikabidhiwa mbegu.
 Hapa wakielekezwa namna ya upandaji wa mbegu hiyo.
  Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Majid Mwanga, akizundua shamba darasa hilo kwa kupanda mbegu.
 Ofisa Kilimo wa Mkoa wa Pwani, Kapilima George na Ofisa Kilimo Ushirika na Umwagiliaji wa Wilaya ya Bagamoyo, Mary Kisimbo wakipanda mbegu hiyo.
Mbegu hiyo ikipangwa katika shamba darasa eneo la Zinga.

Na Dotto Mwaibale, Bagamoyo

MKOA wa Pwani umepokea mbegu bora ya mahindi aina ya Wema kutoka Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) kupitia Jukwaa na Bioteknolojia kwa Maendeleo ya Kilimo (OFAB) kwa ajili ya kupandwa kwenye mashamba darasa mkoani humo.

Akizungumza wakati akipokea mbegu hiyo wakati wa uzinduzi wa shamba darasa uliofanyika jana katika Kijiji cha Kilemela Kata ya Kerege wilayani Bagamoyo Mkuu wa wilaya hiyo Majid Mwanga alisema mbegu hiyo itasaidia kuondoa changamoto ya kupata mbegu bora kwa wakulima wilayani mwake.

"Niwashukuru wenzetu wa COSTECH na OFAB kwa kutukumbuka kwa kuendesha program hii ya kugawa mbegu bora ya mahindi katika mkoa wetu hususan kwenye wilaya yangu ya Bagamoyo" alisema Mwanga.

Alisema mradi huo utasaidia kuongeza ari ya kilimo cha mahindi kwenye wilaya hiyo na kuunga mkono jitihada za Rais Dk.John Magufuli za kuhimiza kufanya kazi kwa bidii na kuanzisha viwanda hapa nchini.

Aliwaomba wakulima hasa kwa wanavikundi waliopata mbegu hizo kuhakikisha wanayatunza mashamba darasa hayo kwa manufaa ya wakulima wote wa wilaya hiyo.

Ofisa Kilimo wa Mkoa wa Pwani Kapilima George alisema mbegu hizo zitaongeza mazao ya mahindi kwani licha ya kutumia mbegu zingine mkoa huo kwa mwaka jana ulipata tani 110.
  

Akizungumza kwa niaba ya  Mkurugenzi Mkuu wa COSTECH wakati wa kukabidhi mbegu hizo, Mkurugenzi wa Fedha wa Fedha na Utawala wa COSTECH, Shabani Hussein alisema kazi kubwa ya COSTECH ni kuishauri serikali katika masuala yote yanayohusu  Sayansi na Teknolojia na kusimamia tafiti zote za kisayansi katika maeneo mbalimbali na kilimo na kuhakikisha zinawafikia walengwa.

Alisema mbegu hizo walizozikabidhi zimefanyiwa utafiti na zitapandwa katika mashamba darasa na baadae kusambazwa kwa wakulima wengine ili kuondoa changamoto ya kukosekana kwa mbegu bora kutokana na wakulima kukabiliwa na mbegu ambazo zilikuwa hazina ubora.

Mtafiti  Kutoka Kituo cha Utafiti wa Kilimo cha Ilonga mkoani Morogoro, Nikidadi Hamidu alisema iwapo mkulima atafuata ushauri wa upandaji wa mbegu hiyo ya Wema 2109 katika ekari moja atapata magunia 35 tofauti na mbegu nyingine ambapo wanapata chini ya hapo.

Ofisa mradi huo kutoka COSTECH, Bestina Daniel alisema kwa mkoa huo wametoa mbegu kilo 58 kwa ajili ya mashamba darasa katika wilaya ya Bagamoyo na Chalinze ambapo kwa wakulima mmoja mmoja wametoa kilo 42 pamoja na mbolea ya kupandia.

Wednesday 14 March 2018


                       
                                    YUNUS HUSSEIN  {ALIYEPOTEA}

MTOTO  YUNUS HUSSEIN PICHANI JUU MWENYE UMRI WA MIAKA 12 AMEPOTEA  NYUMBANI KWAO TOKEA TAREHE 8 MPAKA SASA HAJAONEKANA.
 HIVYO KWA YEYOTE ATAKAE MUONA MAHALA POPOTE ATOE TAARIFA KWA NAMBA ZIFUATAZO 0655090202/ 0655141464/ 06585000510
 AU ATOE TAARIFA KATIKA KITUO CHOCHOTE KILICHOPO KARIBU YAKE- MTOTO YUNUS ANAISHI MBEZI JUU JIJI DAR ES SALAAM NA RB NO NI MBJ/RB/236/2018.

Tuesday 13 March 2018

Na Jumia Travel Tanzania


Zimebaki takribani wiki tatu kabla ya sikukuu ya Pasaka kusherehekewa duniani kote, je umeshafahamu utakwenda kupumzika wapi? 

Pasaka ni miongoni mwa sikukuu zinazopendwa na watu wengi kwa sababu husherehekewa kwa takribani wiki moja. Wakati wa sherehe hizi watu huitumia fursa hiyo kwa kufanya mapumziko ya muda mfupi kabla ya kurejea kwenye shughuli zao za kila siku.

Katika kukusaidia sehemu za kwenda kutembelea sikukuu hii, Jumia Travel imekukusanyia hoteli tano za kuvutia zilizopo pembezoni mwa Tanzania ambazo unaweza kwenda kupumzika kipindi cha likizo hii fupi.

Lupita Island Lodge. Ni hoteli ya kuvutia na tulivu inayopatikana kwenye kisiwa kinachomilikiwa na mtu binafsi ndani ya ziwa Tanganyika. Hoteli hii ina kiwanja binafsi cha ndege na boti ambazo huwachukua wageni kutoka nchi kavu mpaka kisiwani. Hii ni sehemu ambayo unapaswa kwenda kwa ajili ya mapumziko kwa sababu hata namna ya muundo wa vyumba na mazingira yake yamewekwa kumpatia mtu utulivu na usiri akiwa mapumzikoni. Miongoni mwa shughuli za kuvutia ukiwa kisiwani hapa ni pamoja na kutembelea kijiji cha wavuvi, kutalii ziwani kwa kutumia boti na burudani za maonyesho ya kiasili kutoka kwa wanakijiji.  

Katuma Bush Lodge. Ikiwa inapatikana kwenye Hifadhi ya Taifa ya Katavi, hoteli hii imejengwa katika mtindo wa kuvutia na kustarehesha kwa kutumia mahema. Eneo hili linatoa wasaa mzuri kwa wateja kutembelea mbuga yenye mandhari nzuri ya uwanda wa Katisunga. Kwa kuongezea, ni sehemu nzuri kwa watalii ambao wangependa kutembelea na kujionea mazingira mapya tofauti na yale waliyokwishayazoea.  

Wag Hill Lodge & Spa. Hoteli ina mazingira tulivu na vifaa vya kisasa, sehemu kwa ajili ya michezo ya watoto na mandhari nzuri ya Ziwa Victoria, inafaa zaidi kwa mapumziko ya kifamilia na watalii wanaotafuta sehemu nzuri ya kustarehe. Inapatikana kwa mwendo wa dakika 30 kwa kuendesha gari kutokea jijini Mwanza.  

Kigoma Hilltop. Ikiwa ni kituo cha kuvifikia kwa wepesi vivutio vya kitalii katika ukanda wa Magharibi, hoteli hii ya kisasa imejengwa mbali kidogo na mji, kwenye eneo kubwa la milima linalotazamana na Ziwa Tanganyika. Ukiwa hotelini hapa utafurahia mandhari nzuri ya kuvutia ya Ziwa Tanganyika, lenye sifa ya urefu na kina kirefu Afrika na duniani, kutoka kwenye kila chumba. Shughuli za kitalii zipo lukuki mkoani Kigoma kama vile safari za boti ziwani, kupiga mbizi ziwani, kutalii miji ya kihistoria ya Ujiji na Livingstone pamoja na safari ya siku nzima ya kutembelea Hifadhi ya Taifa ya Gombe.   

Kungwe Beach Lodge. Ni hoteli ya kifahari yenye ufukwe wa kuvutia inayopatikana kwenye Hifadhi ya Taifa ya Milima ya Mahale. Ukiachana na mazingira tulivu na vyakula mbalimbali, mgeni anaweza kufurahia shughuli kama vile ziara ya kwenda kuwaona sokwe, kutazama ndege wa mwituni, kutalii mbugani, safari ya boti ziwani, uvuvi, pamoja na matembezi binafsi kwenye fukwe safi pembezoni mwa Ziwa Tanganyika.

Maeneo ya kutembelea ni mengi na yanafikika kwa urahisi zaidi na gharama nafuu endapo utaanza kufanya maandalizi mapema. Sikukuu zinakaribia, naamini miongoni mwenu mtakuwa na mapumziko mafupi. Hivyo ni vema kukitumia kipindi hiko kufanya kitu ambacho kitaacha kumbukumbu katika mwaka huu. Unaweza kufahamu mengi zaidi juu ya sehemu hizo kupitia mtandao wa Jumia Travel.

SPORTS UPDATE

Elimu

NENO

MAKALA

SIASA

DINI

CHEKA

BURUDANI