Showing posts with label siasa. Show all posts
Showing posts with label siasa. Show all posts

Monday, 19 March 2018

 Naibu Katibu Mkuu Wazazi ccm Tanzania bara
Godfrey Mheluka akiwa anawahutumia wananchi waliouthuria katika
kongamano la kujadili maadili mema   na uzalendo  ni ustawi wa Arusha
yetu na Taifa letu  kwa ujumla ,kongamano lililoandaliwa na Jumuiya ya
Wazazi ya Chama cha Mapinduzi (CCM)mkoa wa Arusha ,kongamano ambalo
lilishirikisha wananchi ,viongozi wa dini ,vyombo vya usalama pamoja
na viongozi mbalimbali wa serikali pamoja na wa sekta binafsi
iliyofanyikia katika ukumbi wa Triple A uliopo ndani ya jiji la Arusha
kamanda wa vijana  UVCCM mkoa wa Arusha  Philemon
Molel maarufu kama Monabani akiongea na wananchi waliouthuria katika
kongamano la kujadili maadili mema   na uzalendo  ni ustawi wa Arusha
yetu na Taifa letu  kwa ujumla ,kongamano lililoandaliwa na Jumuiya ya
Wazazi ya Chama cha Mapinduzi (CCM)mkoa wa Arusha ,kongamano ambalo
lilishirikisha wananchi ,viongozi wa dini ,vyombo vya usalama pamoja
na viongozi mbalimbali wa serikali pamoja na wa sekta binafsi
iliyofanyikia katika ukumbi wa Triple A uliopo ndani ya jiji la Arusha
Habari picha na  Woinde Shizza,Arusha
Wazazi wametakiwa kutimiza wajibu  wao wa kuwalea watoto  kwakufuata
maadili ya Mtanzania na kuacha kuiga tamaduni  za kigeni  ,kwani
baadhi ya tamaduni za kigeni wanazo ziiga zinachangia kusababisha
mporomoko wa maadili katika jamii zetu .
Hayo yamebainishwa na Naibu Katibu Mkuu Wazazi ccm Tanzania bara
Godfrey Mheluka wakati akifunga kongomano  la kujadili  maadili mema
na uzalendo  ni ustawi wa Arusha yetu na Taifa letu  kwa ujumla
,kongamano lililoandaliwa na Jumuiya ya Wazazi ya Chama cha Mapinduzi
(CCM)mkoa wa Arusha ,kongamano ambalo lilishirikisha wananchi
,viongozi wa dini ,vyombo vya usalama pamoja na viongozi mbalimbali wa
serikali pamoja na wa sekta binafsi iliyofanyikia katika ukumbi wa
Triple A uliopo ndani ya jiji la Arusha

Alisema kuwa  wazazi wengi wa wamekuwa wanalea watoto kwa kufuata
tamaduni za wenzetu wan chi za nje wakidai kuwa ndio malezi bora kwa
watoto na yakisasa kitu ambacho sio kizuri kwani baadhi ya tamaduni za
wenzetu ukiangalia za kutoka nchi za kimagharibi  zinaporomosho
maadili kwa watoto wetu.
“ukithamini tamaduni za kimagharibi na ukaacha za kwetu na ukamuacha
mtoto nae akathamini tamaduni hizohizo ujue umempoteza mtoto na
umemuaribu kabisa unakuta mzazi anaona mtoto anavaa mlegezo au kimini
badala ya kumkataza anamuacha anaona kuwa wake ndio mjanja huo sio
ujanja ni ujinga ni kumuaribu mtoto unatakiwa umwambie mtoto hivi sio
vyema ivi nikiwauliza wazazi ivi nyie mngelelewa hivyo  au mngelelewa
vibaya je leo mngekuwepo apo mlipo  ni wajibu wetu kuwalea watoto wetu
kwa kufuata utamaduni wetu mzuri wenye maadili ili kuweza kuandaa
viongozi wazuri wa baada na wazazi wazuri wa baadae “alisema Mhekuka

Kwa upande wake mwenyekiti wa jumuiya ya  wazazi ccm mkoa wa Arusha
Dr,John Palanjo alisema ni wazazi anatakiwa kutimiza waji wake kwa
mtoto wake huku pia mtoto akitakiwa kutimiza wajibu wake kwa mzazi
,aliongeza kuwa pia niwajibu wa kila mzazi kumfatilia mtotowake na
kujua maendeleo yake mwenyewe na sio kumuachia mwalimu amfatilie au
dada wa kazi amfatilie huku akibainisha kuwa mzazi yeyote asitafute
mchawi wa mtoto wake kwani ,asilimia kubwa ya wazazi wao wenyewe ndio
wachawi wawatoto wao.
Aidha aliwaasa wazazi kutenga mda wa kukaa na watoto wao na kuongea na
kuwaelezea kipi kibaya na kipi kizuri ili kuwawezesha watoto wetu
kukuwa  kwa kuendana  na yale   yanayopendeza kwa jamii inayowazunguka
.

“mimi na imaini iwapo mzazi akijua wajibu wake atakubali hata kidogo
mtoto wake aharibike ,hivyo ni vizuri mzazi utambue  wajibu  wako
umrudie mungu  usali maana ukiwa na hofu ya mungu lazima utamlea mtoto
kwa kufuata kanuni za kimungu”alisema katibu wa  wawazazi wilaya ya
Arusha Christoper Pallangyo

Kwa upande wake mwenyekiti wa wazazi wilaya  ya Arusha Ally Meku
aliwataka baadhi ya wazazi   kupunguza migogoro  ndani ya familia ili
watoto nao wasiige tabia mbaya kwani  wanapoaanza migogo katika
familia wanashindwa kuwale watoto wao na badala yake watoto hao
wanaanza kutangatanga hovyo na kuanza kuiga tabia mbaya.
 baadhi ya viongozi wakiwa wanaimba na kucheza

 baadhi ya viongozi wakiwa meza kuu wanafatilia kongamano
 RTO  wa mkoa wa Arusha Josephy Bukombe nae alikuwepo katika kongamano hilo ambapo aliwasisitiza wazazi na vijana waliouthuria katika kongamano hilo kufuata maadili ,huku akiwasihi wazazi  kuwakumbusha vijana wao kuvaa kofia ngumu wakati wanapoendesha pikipiki zao pamoja na kufuata sheria za usalama barabarani ili kupunguza ajali ambazo zinaweza kutokea mara kwa mara
 mkuu wa wilaya ya Arusha akiongea na wananchi waliouthuria katika kongamano hilo
 wanafunzi wa shule ya sekondari ya Edmond Rice nao waliuthuria katika kongamano hilo


  mwenyekiti wa jumuiya ya  wazazi ccm mkoa wa Arusha
Dr,John Palanjo akiongea na wananchi waliouthuria katika kongamano hilo

Tuesday, 13 March 2018

 Mjumbe wa halmashauri kuu ya taifa ya chama cha mapinduzi (CCM) MNEC Salimu Asas akiongea na wajumbe wa baraza la UWT manispaa ya Iringa lilofanyika katika ukumbi wa CCM sabasaba na kutoa jumla ya shilingi milioni
kumi na tatu(13,000,000) kwa UWT Iringa Mjini
 Mjumbe wa halmashauri kuu ya taifa ya chama cha mapinduzi (CCM) MNEC Salimu Asas akipokea zawadi kutoka kwa viongozi wa UWT manispaa ya Iringa
 Mjumbe wa halmashauri kuu ya taifa ya chama cha mapinduzi (CCM) MNEC Salimu Asas akibadilisha mawazo na mwenyekiti wa UWT manispaa ya Iringa Ashura Jongo pamoja na mbunge wa viti maalum mkoa wa Iringa Ritta Kabati.

Na Fredy Mgunda,Iringa.

MJUMBE wa halmashauri kuu ya taifa ya chama cha mapinduzi (CCM) MNEC Salimu Asas ameendelea kuineemesha jumiya ya umoja wa wanawake mkoa wa Iringa (UWT) kwa kutoa kiasi cha shilingi milioni nne (4,000,000) kwa jumuiya hiyo wilaya ya Iringa Mjini kwa ajili ya kuendeleza miradi ya umoja huo na kuondokana kuwa tegemezi.
 
Pesa hizo zimetolewa wakati wa baraza la umoja wa wanawake wilaya ya Iringa Mjini mkoani (UWT) lilofanyika katika ukumbi wa chama cha mapinduzi ulipo Iringa Mjini na kuhudhuriwa na wageni wengi wakiwepo wabunge wa viti maalum ambao ni Ritta Kabati na Rose Tweve

Akizungumza katika baraza hilo MNEC Asas alisema kuwa amependezwa na mikakati ambayo imefanya na umoja huo wa wilaya ya Iringa Mjini kwa kuwa wanafanya kazi na viongozi pamoja na wananchi wa chini hivyo inakuwa rahisi kuendelea kukijenga chama hicho.

Nimeona kwenye hotuba yenu mmesema kuwa “mtahakikisha kuwa wanawake wanajiunga kwenye vikundi vya uzalishaji kama vile vikoba ,saccos na vikundi vingine ili waweze kupata mafunzo stahiki ya ujasiliamali kwa lengo la kupambana na hali ya kiuchumi na kuongeza kipato,”hakika kwa kufanya hivi mtawaokoa wanawake wengi sana kiuchumi. Alisema Asas 

Asas alisema kuwa nimesikia mnataka kuanzisha duka kwa ajili ya kuongeza ajira na kuongeza uchumi wa umoja huu,hilo ni jambo bora hivyo kwa kuona mikakati hiyo nawachangia kiasi cha shilingi milioni nne (4,000,000) ili wafikie malengo ya kujiendesha na kuacha kuwa tegemezi.

Aidha Asas alimpongeza mbunge wa viti maalum mkoa wa Iringa Rose Twelve kwa jitihada alizozifanya za kuwawezesha wanawake kiuchumi kwa kutoa mitaji kwenye kata kumi na saba  kwa kutoa kiasi cha shilingi laki sita kwa kila kata,hivyo kwa kuliona hilo MNEC alisema kuwa atachangia kiasi cha shilingi laki tano kwa kila kata hivyo kwa kata zote 18 za wilaya ya Iringa Mjini atachangia kiasi cha shilingi milioni tisa (9,000,000).

Kwa hili sipepesi macho nampongeza sana mbunge Rose Tweve kwa kazi kubwa anayoifanya kuhakikisha wanawake wanapata mafanikio kwa kuwawezesha kama alivyofanya kwa kufanya hivyo amefanikiwa kuwafikia wanawake walio na kipatao cha chini kabisa na nitaendelea kukusaidia mbunge kwa kazi unazozifanya kwa ajili ya maendeleo” alisema Asas

Kwa upande wake katibu wa UWT wilaya ya Iringa Mjini Frola Kapalia alimshikuru MNEC Salim Asas kwa kutoa msaada mkubwa kama huo ambao hata wao hawakutegemea kutokea kitu kama hicho,ambapo ukipiga mahesabu utagundua kuwa ametoa jumla ya shilingi milioni kumi na tatu(13,000,000) kwa UWT Iringa Mjini

“Ametoa shilingi mioni nne kwa UWT na ametoa milioni tisa (9,000,000) kwa ajili ya kuongezea nguvu kwenye mfuko wa mbunge Rose Tweve hivyo lazima tujivunie kuwa na MNEC wa namna hii” alisema Kapalia

Thursday, 8 March 2018

 Mwenyekiti wa Umoja wa wanawake Tanzania (UWT) Gaudentia Kabaka akifurahia mtoto wa kike, alipotembelea wodi ya Wazazi katika Hospitali ya Mbaala Rangi tatu, wilayani Temeke Dar es Salaam, ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Siku ya Mwanamke Duniani, leo Machi 8, 2018. Mapema Mama Kabaka akiambatana na kina mama mbalimbali wakiwemo viongozi wa UWT kutoka maeneo mbalimbali, alishiriki kufanya usafi na baadaye kutoa zawadi mbalimbali kwa uongozi na waonjwa kwenye Hospitali hiyo. Kulia ni Mariam Salum, mzazi wa mtoto huyo. 
 "Haya Mama chukua kichana chetu.." akasema Mama Kabaka wakati akirejesha mtoto kwa Mariamu Salum baada ya kumkabidhi zawadi ya kanga.
 Mama Gaudentia Kabaka akitoa zawadi za juisi kwa kina mama waliojifungua katika hospitali hiyo ya Mbagala Ranitatu
 Baadhi ya Kinamama wakaiwa na zawadi za kanga na sabuni ambazo Mama Kabaka aliawa kwa kina amama waliojifunua katika hospitali hiyo.
 "Hebu chukua kanga hii kutoka kwa kina mama wenzako.." akasema Mama Kabaka wakati akimkabidhi Mwajuma Ally aliyejfungua mtoto katika hospitali ya Mbagala Rangitatu
 "Loooh mtoto umejifunugua mtoto mzuri sana..." akasema Mama Kabaka 
 Kisha akampatia zawadi ya mche wa sabuni
 Diwani wa Viti Maalum CCM, Mariam Mtemvu na wenzake wakimsalimia mmoja wa Kina mama aliyekuwa katika Wodi ya Wazazi baada ya kujifungua katika hospitali ya Mbagala Ranitatu, leo
 Ofisa wa Makao Makuu ya UWT Ndugu Kisa wapili kulia, akiwa na kina mama weningine.
 Ofisa wa Makao Makuu ya UWT Ndugu Kisa (kushoto), akiwa na wauguzi na kina mama weningine kwenye hospitali hiyo ya Mbagala Ranitatu leo. 
 Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Gaudentia Kabaka akimpa zawadi ya kanga mmoja wa wauuzi katika hospitali ya Mbagala Rangitatu wakati wa ziara hiyo
 "Wauuzi na Madaktari honereni kwa kazi nzuri na hasa kwa kujali afya za kina mama na watoto...endeleni kuchapa kazi tupo pamoja nanyi", alisema Mama Kabaka wakati akizunumza na baadhi ya wauguzi na madaktari wa hospitali ya Mbagala Ranitatu wakati wa ziara hiyo. Kushoto ni Matroni wa wodi ya Wazazi Maria Lumambo
 Mama Kabaka akiendelea kuzunumza nao
 Mweneyekiti wa UWT Gaudentia Kabaka akifuatana na Matroni wa Wodi ya Wazazi Maria Lumambo, baada ya kutoka wodini kuwaona na kuwapa zawadi wazazi
 Mweneyekiti wa UWT Gaudentia Kabaka akizungumza baada ya kutoka wodini kuwaona na kuwapa zawadi wazazi
 Picha ya kumbukumbu
Mweneyekiti wa UWT Gaudentia Kabaka akiwa tayari kuondoka kwenye Hospitali ya Mbagala Rani tatu baada ya ziara yake leo. PICHA ZOTE NA BASHIR NKOROMO

Saturday, 3 March 2018


Watu wawili wamekatwa na kufungwa jela baada ya kumchezea rafu Rais wa Burundi, Pierre Nkurunzinza katika mchezo wa kirafiki uliokuwa dhidi ya timu yake na wapinzani.

Nkurunzinza ambaye alikuwa na kikosi chake cha Haleluya FC, Februari 3 2018 walikuwa wakicheza mchezo wa kirafiki dhidi ya Kimbere FC iliyopo Kaskazini mwa nchi hiyo ya Burundi.

Katika mchezo huo, Kiremba FC ilikuwa na wachezaji ambao baadhi ni wakimbizi kutoka Congo waliokuwa hawajui kama wanacheza na Rais wa Burundi hivyo walikuwa wakimchezea rafu kila muda.

Kitendo cha kumchezea rafu Rais huyo, kilichukuliwa kama njama za kutaka kuhatarisha afya ya Rais Nkurunziza hivyo Serikali ikachukua maamuzi ya kuwafunga jela.

cHANZO : SALEH JEMBE BLOG

Monday, 18 December 2017

 Mwenyekiti wa CCM Rais Dk. John Magufuli akifungua Mkutano Mkuu wa tisa wa CCM, katika Ukumbi wa Jakaya Kikwete, Dodoma, leo. Pamoja na mambo mengine kuhusu mageuzi ndani ya Chama, uadilifu na usimamizi wa mali za Chama ili Chama kisitegemee wafadhili wakiwemo matajiri wachache, amemtaka Katibu Mkuu wa CCM, Ndugu Abdulrahman Kinana kuendelea kumsaidia katika nafasi hiyo ya Katibu Mkuu katika kipindi kingine cha miaka mitano
 Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akimsalimia Balozi wa China hapa nchini Wang Ke, alipokuwa akisalimia mabalozi kutoka nchi mbalimbali ambao wamehudhuria Mkutano huo 
 Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana na Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara Rodrick Mpogolo wakikagua mazingira ya nje ya ukumbi kabla ya mkutano huo mkuu kuanza
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Humphrey Polepole akiandaa mazingira ya kuchangamsha ukumbi kabla ya mkutano huo kuanza. Kushoto ni katibu wa NEC Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Kanali Mstaafu Ngemela Lubinga
 Wanakwaya wa TOT wakiimba wimbo maalum wa kumkaribisha ukumbini Mwenyekiti wa CCM, Rais Dk John Magufuli
 Wajumbe wakijimwayamwaya ukumbini kushangilia wakati Mwenyekiti wa CCM Taifa, akiingia ukumbini
 Mwimbaji wa TOT akiimba wimbo wa kuhamasisha mapokezi ya Mwenyekiti ukumbini
 Mwenyekiti Mstaafu wa CCM Jakaya Kikwete na Mwenyekiti mstaafu wa CCM Ali Hassan Mwinyi wakimsubiri Mwenyekiti Kuingia Ukumbini. Mzee Mwinyi akisoma toleo maalum la gazeti la Uhuru wakati akisubiri
 Viongozi waliotangulia meza kuu wakisimama kumlaki Mwenyekiti wa CCM rais Dk John Magufuli wakati akiingia ukumbini
 Mwenyekiti wa CCM Rais Dk John Magufuli akisalimia viongozi mbalimbali baada ya kuingia ukumbini. Kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa CCM, Rais wa Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein na kulia ni Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana
 Mwenyekiti wa CCM Rais Dk John Magufuli akiwa tayari ukumbini. Wengine kushoto ni Mwenyekiti wa CCM Mstaafu Jakaya Kikwete, Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan, Makamu Mwenyekiti wa CCM Rais wa Zanzibar Dk. Shein, Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana, Makamu Mwenyekiti wa CCM-bara Philip Mangula na Mwenyekiti Mstaaafu wa CCM Benjamin Mkapa
 Mwenyekiti wa CCM Rais Dk John Maguduli akijadili jambo na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Kinana baada ya kuketi ukumbini
 Waimbaji wa TOT wakiimba wimbo wa Taifa kabla ya Mkutano kuanza
 Wajumbe wakiwa wamesimama kuimba wimo wa Taifa
 Mwenyekiti wa CCM Rais Dk John Magufuli na viongozi wengine meza kuu wakiimba wimbo wa Taifa huku wamesimama kwa ukakamavu 
 Viongozi wakiw wameketi baada ya kuimba wimbo wa taifa
 Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akiondoka meza kuu kwa ukakamavu kwenda kufuatilia jambo
 Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akimkaribisha Mwenyekiti kufungua Mkutano huo
 Wapicha picha wakifuatilia matukio
 Mjane wa Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere Mama Maria Nyerere akiwa na Mama Salma Kikwete kwenye mkutano huo
 Baadhi ya wageni waalikwa na wajumbea wakiwa kwenye mkutano huo
 Mwenyekiti wa CCM Rais Dk Magufuli (kulia)akifungua mkutano huo mkuu
 Wajumbe wakishangilia baada ya Mwenyekiti wa CCM Rais Dk Magufuli kumtaka Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana kuendelea kumsaidia katika nafasi hiyo ya Ukatibu Mkuu kwa miaka mingine mitano
 Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akionekana kutafakari baada ya kauli ya Mwenyekiti wa CCM Dk Magufuli  kumhitaji tena
 Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akiinuka kuonyesha ishara ya kukubali makakwa ya Mwenyekiti wa CCM Rais Dk. Magufuli. Kulia ni Mwenyekiti Mstaafu wa CCM Zanzibar Dk Amani Abeid Karume na Mzee Mkapa ambaye anacheka kuonyesha kuunga mkono
 Baadhi ya waliohamia CCM kutoka vyama vya upinzani wakisimama baada ya kutmbulishwa na Mwenyekiti wa CCM Rais Dk Magufuli kwenye mkutano huo