Tuesday 2 February 2016

TAARIFA KWA UMMA KUFUTA USAJILI WA SHIRIKA LA APOPA

By    
Taarifa inatolewa kwa umma kwamba Bodi ya Uratibu wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali katika kikao chake cha 38 kilichofanyika tarehe 27 Januari, 2016 iliazimia kufuta usajili wa Shirika la African Poor and Patient Organization (APOPA) kutokana na kukiuka masharti ya Sheria ya NGOs Na. 24 ya mwaka 2002 (kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2005).

Kwa taarifa hii, shughuli za Shirika tajwa zimekoma kuanzia tarehe ya ttangazo la taarifa hii. Wanachama wa shirika wanaagizwa kusitisha shughuli za shirika na kuzingatia taratibu za ufungaji wa shughuli za Shirika kama zinavyoainishwa katika katiba ya Shirika na Kanuni za Sheria ya NGOs, GN.Na.8 ya Mwaka 2015.

M.S.Katemba
MSAJILI WA NGOs
2 Februari, 2016

0 comments