Tuesday 19 July 2016

DC MUHEZA AWATAKA WAFANYABIASHARA WA SOKO LA SAMAKI KUHAMIA ENEO LA SOKO LA MICHUNGWANI

By    
Mkuu wa wilaya ya Muheza Mkoani Tanga,Hajat,Mhandisi Mwanasha Tumbo kulia akizungumza na wafanyabiashara wa samaki katika soko la kuuzia samaki wabichi na wakavu ambalo limevunjwa na kutakiwa kuhamia kwenye soko la michungwani ambalo limejengwa kwa ubora kwa ajili ya kufanya shughuli zao

Mfanyabiashara wa soko la samaki la  kulia akimuonyesha mkuu wa wilaya ya Muheza,Hajat,Mhandisi Mwanasha Tumbo kitu wakati alipotembelea soko la kuuzia samaki wabichi na wakavu ambapo aliwataka wafanyabiashara hao kuondoka eneo hilo kuhamia eneo la michungwani.

Mkuu wa wilaya ya Muheza Mkoani Tanga Hajat,Mhandisi Mwanasha Tumbo akisisitiza jambo kwa wafanyabiashara wa soko la samaki wabichi na wakavu kuhusu kuondoka eneo hilo na kuhamia soko la michungwani ambalo limejengwa kwa ubora mzuri kwa ajili ya kufanyia biashara zao

Mkuu wa wilaya ya Muheza Mkoani Tanga Hajat,Mhandisi Mwanasha Tumbo kulia akimsikiliza mmoja wa wafanyabiashara ya samaki katika soko la kuuzia samaki wilayani humo ambao waliamuriwa kuhamia kwenye soko la Michungwani ambalo limejengwa kwa ubora kwa ajili ya shughuli zao.
Habari kwa Hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha

0 comments