Wednesday 29 January 2014

MAVAZI YASIYO RUHUSIWA KATIKA OFSI ZA WATUMISHI WA UMMA

Wizara ya utumishi wa umma imetuma waraka unaotoa mwongozo wa mavazi kwa watumishi wote wa ofisi za umma na wananchi wote wanaohitaji huduma ktk ofs hizo.


Waraka huo namba 3 wa mwongozo wa mavazi wa mwaka 2007 unawatka wafanyakazi wote wa ofisi za umma na wananchi wote kutokuvaa mavazi yafuatayo:-
-Jeans
-Nguo zenye maandishi yoyote
-Nguo zinazobana mwili wako
-Nguo zilizo juu ya magoti (sketi/gauni)
-Kaptula
-Pedo
-Jezi za timu za mpira
-Nguo za chama chochote cha siasa
-Suruali ambazo hazijapindwa
-Blauz zinazoacha kifua/mgongo wazi
-Kuvaa mlegezo


Waraka huo ulikuwepo ila uekelezaji haukufanyika,hivyo kwanzia mwaka huu utaanza kutumika nchi nzima.


Wananchi usiende ofisi za umma ukiwa umevaa mavazi tajwa hapo juu,utaishia kufukuzwa bila kuhudumiwa...

0 comments