Friday 24 October 2014

KITUNGUU SWAUMU NI KIUNGO NA NI DAWA YA MARADHI ZAIDI YA 30

By    
Kitunguu swaumu hakikosekani katika kila jiko duniani.Ni mmea maarufu sana kwa tiba.Kitunguu swaumu ni jamii ya yungiyungi.

Kitunguu swaumu kilicho bora zaidi duniani ni kinachotoka misri kwasababu ya tabia ya ardhi yake na mto nail.

Kitunguu swaumu kina harufu ya kipekee isiyowapendeza watu wengi ingawa kimebeba siri nyingi za tiba. Kwa ajili hiyo maana yake kilatini ni HARUFU ICHOMAYO.
Ili kuepukana na harufu ya kitunguu swaumu baada ya kukila,kula tofaa au tafuna majani mabichi ya naanaa,au kunywa maji yaliyotokosewa karafuu.
Kitunguu swaumu kitapoteza nguvu ya tiba iwapo kitapikwa na kila kinapowekwa muda mrefu ndipo nguvu zake huongezeka (baada ya majani yake kukauka kabisa).
Kitunguu swaumu kimekusanya protin 49%,sulphur 25%,kiasi fulani cha chumvi,homoni zitoazo nguvu za kiume,viuaji sumu,vikojozavyo,vitoavyo safura,vinavyoteremsha hedhi,vimeng'enyo vyenye kuyeyusha mafuta na viini vyenye kuua minyoo.
Kila utafiti unapoendelea ndipo faida na maajabu ya kitunguu swaumu yanapoongezeka.

BAADHI YA MARADHI YANAYOTIBIWA NAKITUNGUU SWAUMU;

1.Kiua sumu
2.Kisafisha tumbo
3.Kiyeyusha mafuta(cholestr
o)
4.Huzuia mvilio wa damu
5.Kusafisha njia ya mkojo
6.Kutibu amoeba
7.Kuzuia kuhara damu(Dysentery)
8.Tumbo kushindwa kumeng'enya(Indigestion)
9.Gesi
10.Msokoto wa tumbo
11.Typhoid
12.Kidonda kilichooza
13.Dondakoo
14.Mabaka
15.Baridi yabisi(Rheumatisim)
16.Mishipa
17.Uziwi
18.Virusi vya homa ya mafua(Influenza
19.Mafua
20.Saratani(Can
cer)
21.Kifaduro
22.Kifua kikuu cha mapafu
23.Kipindupindu
24.Kutoa minyoo
25.Upele
26.Kuvunjavunja mawe katika figo
27.Mba kichwani
28.Kuupa nguvu ubongo
29.Kuupa nguvu fizi
30.Kuzuia meno kung'ooka
31.Nguvu za kiume
32.Maumivu ya kichwa
33.Kizunguzungu/kisunzi
34.Kutuliza maumivu ya meno
35.Kujenga misuli na kutia nguvu
36.Mkakamo wa ateri(Arteriosclerosis)
37.Shinikizo la damu
38.Kinga ya tauni na ukimwi
39.Magonjwa ya macho

MATUMIZI NA MAANDALIZI KATIKA KUTIBU

Matumizi na maandalizi ya kitunguu swaumu katika tiba yanategemea aina ya maradhi unayotaka kuyatibu,hivyo basi ni muhimu kuwasiliana na wataalamu wa tiba mbadala ili uweze kupata maelekezo sahihi ya namna ya kuandaa kulingana na ugonjwa unaokusumbua.
Kumbuka kama tulivyosema awali kuwa kitunguu swaumu kikipikwakinapoteza nguvu ya tiba kutegemeana na tiba unayokusudia.
Kumbuka pia kwamba kitunguu swaumu huweza kuchanganywa na vitu vingine mfano;maziwa,asali,habatsouda,juisi,shayiri n.k. kutegemea na maradhi unayotaka kuyatibu na kwa ushauri/maelekezo ya daktari.

0 comments