Monday 22 December 2014

MGOMI: UTOAJI WA ELIMU YUARAHISIHA UFIKAJI WA NISHATI VIJIJINI

By    
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgUytMJMSyYWS4ThNO1cfmiK1K9WLusofw6d-ARy7PzGIp1NQIEml0aB5YzTuM-Z23NAAWtB9PQO1qKU8kz3M-sjyMWTVMHxDCu4bY4WnGcJOnDUmaeMxF4qhZBtcsKb3rhROu-fphdSOU/s1600/SAMAKI.JPG
Jitihada za kutoa elimu kwa jamii zinazoendelea kutolewa kupitia wakala wa nishati ya umeme vijijini huenda itasaidia kukabiliana na uharibifu wa mazingira ya bahari na kufanikisha malengo ya mkukuta ya kufikisha nishati vijijini itafanikiwa ifikapo mwaka 2015.

Mkuu wa wilaya ya Masasi Farida Mgomi amesema hayo mjini Masasi wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya ukaushaji wa samaki kwa kutumia nishati ya jua yaliyoshirikisha washiriki 20 kutoka Somanga wilaya ya Kilwa mkoani Lindi ambapo ametaka mafunzo hayo kuchangia kuboresha shughuli za uvuvi kwenye maeneo ya bahari ya Hindi na hivyo hivyo kukuza soko la samaki na kuchangia katika maendeleo ya jamii na kupunguza umaskini wa kipato.

Mratibu wa mafunzo hayo FRED MWAKAGENDA amesema mafunzo hayo yana lengo la kusaidia uboreshaji wa kukausha samaki na kupunguza uharibifu wa mazingira pamoja na kuongeza ushindani wa soko kwa wajasiliamali.

0 comments