Shirika la kuzuia la Umoja wa Mataifa linaloongoza harakati dhidi ya
Ukimwi, UNAIDS nalo limepaza sauti dhidi ya muswada wa sheria wa kupinga
mapenzi ya jinsia moja nchini Uganda likisema ukiwa sheria utasababisha
ongezeko la maambukizi ya virusi vya Ukimwi na kinyume na haki za
binadamu.
Mkurugenzi Mtendaji wa UNAIDS, Michel Sidibé amesema
Uganda ilikuwa nchi ya kwanza ya kiafrika kuvunja mipaka na kujumuisha
makundi ya pembezoni katika kukabiliana na ukimwi lakini sheria hiyo
sasa itatumbukiza kapuni mafanikio yote yaliyopatikana.
Ameitaka serikali ya Uganda kutupilia mbali muswada huo akieleza kuwa
utakuwa na madhara kwenye afya ya kijamii kwani utafiti umeonyesha kuwa
mashoga wanapobaguliwa, wanakuwa na hofu kusaka huduma za kinga au tiba dhidi ya Ukimwi.
Chanzo:Ahbaabur



0 comments