Wednesday 22 October 2014

MAJI NI TIBA YA MARADHI MENGI

By    
Hamuwezi kuamini! maradhi mengi Mwenyezi Mungu amejaalia tiba yake ni kunywa maji, shukrani zote ni zake..
Umoja wa Matabibu wa Japan wametangaza utafiti wao wa kutibu maradhi kwa maji na matokeo yake yamefanikiwa kwa aslilimia 100, kwa maradhi yafuatayo:


kichwa, presha, anaemia (upungufu wa damu) ugonjwa wa viungo, kupooza, kuzima kwa moyo, kifafa,unene, kikohozi, kuumwa koo, pum, kifua kikuu,uti wa mgongo, na mradhu yeyote yanayohusiana na njia za mkojo, asidi nyingi,kufunga choo,na maradhi yote yanayohusiana jicho, sikio na koo, pia kwa wanawake wasiopata ada ya mwezi kwa mpangilio

Njia ya kutibu kwa maji

Amka mapema asubuhi kila siku na kunywa glasi nne(4) za maji, glasi ya kiasi cha mil 160. Kunywa wakati tumbo halina kitu na wala usile wala usinywe kabla ya kupita dakika 45 , na usile wala usinywe masaa mawili yanayofuatia chakula

Kuna baadhi ya watu au wagonjwa na wazee hawataweza kunywa glasi nne za maji kwa wakati mmoja, hawa wanaweza wakaanza kidogo kidogo huku wakiongeza kunywa mpaka wafikie kiwango kilichopendekezwa kwa wakati mfupi

Na matokeo yamethibiti kwamba tiba ya maji imeleta ponya na maradhi yafuatayo kwa muda maalum kama inavyoonyeshwa hapa chini: maradhi ya sukari siku 30 kupanda presha siku 30 matatizo ya tumbo siku 10 saratani mbali mbali miezi 9 kifua kikuu na uti wa mgongo miezi 6 kufunga choo siku 10 matatizo ya njia za mkojo na figo siku 10 matatizo ya pua, sikio na koo siku 20 matatizo ya ada za mwezi kwa wanawake siku 15 matatizo mbali mbali ya moyo siku 30 maumivu ya kichwa siku 3 anaemia(upungufu wa damu) siku 30
unene miezi 4 kifafa na kupooza miezi 9 matatizo ya kuvuta pumzi miezi 4

0 comments