Dk. Bilal alitoa kauli hiyo Jijini Dar es Salaam jana alipokuwa akifungua kongamano la kimataifa la siku tatu la masuala ya uwekezaji wa fedha, miradi na ubia lenye lengo la kupanua fursa za uwekezaji nchini lililoandaliwa na Taasisi za Sekta Binafsi Tanzania (TPSF), wakishirikiana na Kampuni ya Kukuza Mitaji ya TMS Consultants.
“Tuna changamoto ya mitaji hasa kwa wafanyabiashara wetu, kwa hiyo tunaweza kutumia fursa hii ya uwekezaji wa hisa kama mtu una kampuni au ubunifu utaweza kujipatia mtaji wa kuiendeleza biashara yako,” alisema.
“Kwa mfano tuna gesi hivi sasa..lakini mtu hana mtaji wa kuwekeza katika sekta hiyo, hawa wenzetu wamekuja na kiasi kikubwa cha fedha kwa ajili ya kuwekeza, kwanini tusitumie nafasi hiyo?” alihoji Mengi ambaye pia ni Mwenyekiti Mtendaji wa IPP.
CHANZO: TANZANIA DAIMA



0 comments