Tuesday 23 December 2014

RAIS MUGABE ATIMUWA MAWAZIRI

By    
Raisi wa Zimbabwe Robert Mugabe amewafukuza kazi mawaziri wake wawilina manaibu waziri wapatao watano hatua ambayo imemkumba aliyekuwa makamu wake Joyce Mujuru.

Hatua hii ya kuwafuta kazi mawaziri wake inafuatia hali tetet ya kisiasa nchini humo na kujiandaa na lolote litakalo tokea lakini pia ni kutokana na mafanikio hafifu ya kiongozi huyo mwenye umri wa miaka tisini endapo atajiuzulu ama kufa.

Mugambe ambaye siku za hivi karibuni ameamua kupumzika katika msimu huu wa sikuku na kuchagua bara la Asia kupumzika yeye na familia yake.lakini wadadisi wa mambo wanasema mafanikio ya Raisi huyo ambayo ni hafifu hayakutarajiwa na walio wengi.

Hofu ya kupokwa madaraka aliyonayo Rais Mugabe ilimsukuma kumtimua kazi makamu raisi wake bi Jopyce Mujuru aliyekuwa akipata umaarufu mkubwa kisiasa nchini mwake , na ndipo mkewe bi Grace Mugabe ambaye naye amepanda umaarufu kisiasa na hivyo kumtia Joyce kumshauri afanye hivyo.

Mujuru aliingia katika kashfa ya kutaka kumuua raisi,lakini pia anashutumiwa kukigawa chama cha ZANUPF,na linguine kuonekana kushindwa kwa Mujuru kufunga mikataba ya kibiashara

Kufuatia tuhuma hizo nafasi ya bi Mujuru ilichukuliwa na waziri Emerson Mnangwaga mshirika wa miaka mingi wa raisi Mugabe.

CHANZO: BBC SWAHILI

0 comments