BAADHI ya wakazi wa mjini hapa wamepigwa na butwaa kuwaona baadhi ya
maofisa wa polisi wakitembeza bakuli mitaani wakiomba mchango wa fedha
kwa ajili ya ukarabati wa magari mabovu ya polisi.
Mshangao wa wakazi hao unatokana na zoezi linalodaiwa kufanywa na baadhi ya maofisa wa polisi, wanaowatembelea wafanyabiashara mbalimbali mjini hapa wakichangisha fedha wakidai zitasaidia kufanyia matengenezo ya magari mengi ya polisi ambayo ni mabovu kwa kipindi kirefu.
Wakizungumza na waandishi wa habari jana mjini hapa, baadhi ya wananchi walioshuhudia kuchangishwa kwa michango hiyo, walielezea kutoamini walichokiona kwa vile si kawaida kwa taasisi za serikali kutembeza bakuli kuomba michango ya fedha kwa ajili ya kuendeshea shughuli zake za kila siku.
Mshangao wa wakazi hao unatokana na zoezi linalodaiwa kufanywa na baadhi ya maofisa wa polisi, wanaowatembelea wafanyabiashara mbalimbali mjini hapa wakichangisha fedha wakidai zitasaidia kufanyia matengenezo ya magari mengi ya polisi ambayo ni mabovu kwa kipindi kirefu.
Wakizungumza na waandishi wa habari jana mjini hapa, baadhi ya wananchi walioshuhudia kuchangishwa kwa michango hiyo, walielezea kutoamini walichokiona kwa vile si kawaida kwa taasisi za serikali kutembeza bakuli kuomba michango ya fedha kwa ajili ya kuendeshea shughuli zake za kila siku.



0 comments