Wednesday, 28 May 2014

MSUNI KUIWAKILISHA JAVA FC KESHO

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj0Ks2PcJDVU0V_RXhwKIWVkIXCfq7WBTGT_urwl4rhP9HLRLVh0tvJjFMDV0IJ2YofxziW_8fXlbYkvKu_4rf2PMZsw2w6bAifiOtiEJ924wxUbCwOZxi-Y2RgVE8SPLxDpfGKojEicsI/s1600/msuni1.jpg
Msuni 

Mmiliki wa Aboodmsuni Network, Abdallah H.I Sulayman (Msuni) anatarajia kesho kuonekana kwa mara nyingine akicheza mpira wa miguu baada ya kukaa nnje ya uwanja kwa takribani mwaka mzima.
 
Msuni ambaye pia ni mwanafunzi wa mwaka wa mwisho diploma katika chuo cha Al-Maktoum College Of Engineering and Technology akichukuwa fani ya Information tchnology, kesho anataraji kuwa miongoni mwa watakao vaa jezi za wanafunzi wa kitengo chake mwaka wa mwisho watakapo cheza na ndugu zao wa Electrical.

Timu ya wanafunzi wa mwaka wa mwisho diploma wanaochukuwa Information Techonology toka Al-Maktoum College of Engineering (Java FC) watachuana vikali na ndugu zao wa mwaka wa mwisho diploma wanao chukuwa Electrical (High Voltage FC), mchezo utakaochezwa saa nne na nusu asubuhi katika uwanja wa shule ya msingi ya Mbezi beach.

Hii itakuwa ni mara ya kwanza kwa wanafunzi wa Al-maktoum kucheza mechi ya wenyewe kwa wenyewe, ikiwa timu ya chuo teayari imeshawahi kushiriki mashindano matatu na kufanikiwa kutwaa ubingwa mashindano mawili kati ya matatu waliyopata kushiriki.
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiMaZaamhiV5-abVoyOnZrNL8_zl9AQyz_nluSo1SJpOS7i0Ymzdr7Ny46LoWjZCcv0yQvOfEP1JmwVVah2V0yuD9YZY33iU0AmX33FaeOTEbGBrR4mfXOfmBvvhNaCUujX6p5cph80arw/s1600/amcet+student.jpg
Baadhi ya Wachezaji wa Java FC wakiwa katika picha ya pamoja
Java FC iko chini ya kocha All Mgweno teyari wamekwisha anika kikosi chao ambacho kinamjumuisha Msuni sambamba na Kaseja wa Tanga Khamisi Abeid.
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgaM2rkGxODYC0yTwfa8xKSFi8oVSvbBOzd45pQw1lCv6KWkOh2sECOUgbzqVwDUmzhtpfObnUooVS9i4bM-6sZMBFhNZv52wtHeVzd0HBKTDp2L6iKMOMY7fsURbycn9u0rzRJ6yBWd5c/s1600/IMG0486A.jpg
Abdallah H.I Sulayman (Abood Msuni)
Wachezaji wengine wa Java FC watakao anza ni pamoja na Rashid Hassan, Ahmada Mohammed, Abdallah Kombo, Sultani Ngaliwata, Suleyman Omari, Ishaka Milandu (mmiliki wa Milandu Sport), Ramadhani Sadick, Mbwana Mohammed na Ramdhani Saidi.
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgLwn15BR-dH9kBuOPiIqH8yYu05du_n0F79jokcuHP-wEk7SIfA-CMTSTvBI4TYx4Y1ngGtTq-Oi21ahvbMXtjx3ActkkC0mjI5zV4Dzc6K4wTzdOJmSN7uG67H96OthlYmOFqdf4Mj6s/s1600/java+fc.jpg
Wakati kikosi cha High Voltage FC kinaundwa na Nuaym, Mussa Kombo, Khalidi, Ammar, Shekhe Shabani, Shabani, Hassan Nondo, Idrissa Kefea na Habibu Lukali.

0 comments