Sunday, 22 December 2013

MARUFUKU KUVAA SKETI FUPI, PICHA ZA NGONO

Bunge la Uganda limepitisha muswada unaopiga marufuku wanawake kuvaa sketi fupi, pamoja na vitendo vinavyochochea ngono, limeripoti gazeti binafsi la Daily Monitor.

Muswada huo uliopendekezwa mwaka 2011 unapiga marufuku pia video za ngono, miziki na hata ngoma zinazochochea vitendo hivyo.

Serikali ya Uganda inasema kuwa, picha za ngono zimekuwa tatizo kubwa kwa jamii na huchochea jinai za ngono dhidi ya wanawake na watoto kama vile kubakwa na kutumiwa watoto wadogo katika ngono.

Kwa mujibu wa sheria hiyo mpya ni marufuku kuacha wazi baadhi ya sehemu za mwili kama vile makalio, mapaja na matiti na kutenda kitendo chochote kinachochoea hisia za ngono.




Chanzo: ahbaabur

0 comments