Monday, 3 February 2014

SHAHNAZ LAGHARI: AWEKA REKODI YA KUWA MWANAMKE WA KWANZA DUNIANI WA KIISLAMU KUENDESHA NDEGE AKIWA NA NIQABU

Shahnaz Laghari ni mwanamke wa kiislamu anayevaa 'baparda' ameweka rekodi na kuingia katika kitabu cha Guiness (Guiness book of world record) kwa kuwa mwanamke wa kwanza duniani wa namna hiyo kuendesha ndege.

Baparda ni aina ya Baibui pana pamoja na Niqabu linakaribiana na Burqa. Shahnaz Laghari ameonesha uwezo wa kurusha ndege peke huku akiwa katika mavazi kamilifu ya stara ya kiislamu.

Shahnaz ambaye mwaka 2013 aliwania ubunge kama mgombea binafsi ameonesha kwamba mtu anaweza kufanya jambo kubwa la kimaendeleo na bado akaendelea kubaki katika mipaka ya dini. 

Rubani huyo ni mtetezi mkuu wa haki za wanawake wa Pakistan. Aidha anajitolea kuwasaidia wanawake wa kwa kufungua vituo vya elimu ya bure na vituo vya kushona kwa ajili ya wanawake maskini katika Pakistan.
akijiandaa kushuka katika ndege
Baada ya kushuka
Akirusha ndege
Ndani ya ndege
Katika harakati za kuwasaidia wanawake wenzake


CREDIT: Ahbaabur Rasuul

0 comments