Jitihada
za mara ya kwanza kwa Sudan Kusini kufuzu kucheza mashindano ya Kombe
la Mataifa ya Afrika zimekatishwa tamaa na kipigo cha magoli 5-0 kutoka
kwa Msumbiji, katika mechi ya duru ya kwanza.
Goli la kwanza lilifungwa na Josimar
Machaisse. aliyefunga kutoka nchani mwa 18 alipounganisha krosi
iliyoingia kutoka upande wa kushoto.
Dakika nne kabla ya mapumziko, mlinzi Mexer
aliachiwa nafasi nje ya eneo la hatari kisha akakung’uta mkwaju wa juu
uliotikisa pembe ya nyavu.
Magoli mengine matatu yalitoka kwa Sonito na Isac Carvalho.
Matokeo ya mechi nyingine ni kama ifuatavyo:-
Madagascar 2 – 1 Uganda
Kenya 1 – 0 Visiwa vya Comoro
Liberia 1 – 0 Lesotho Swaziland 1 - 1 Sierra Leone
Burundi 1 – 1 Botswana
Central African Republic 0 – 0 Guinea Bissau
Libya 0 – 0 Rwanda
0 comments