KIUNGO wa Arsenal, Mikel Arteta amesema
kutwaa Kombe la FA kumesaidia kocha Arsene Wenger kubaki kazini. Wenger
alikaa na klabu hiyo ya London Kaskazini kwa miaka tisa bila taji kabla
ya kutwaa Kombe la FA na kurudisha hali ya utulivu kwa mashabiki.
Arsenal ilifungwa mabao 2-0 na Hull City
katika dakika za kawaida kabla ya kuibuka na kushinda mabao 3-2 katika
dakika za nyongeza kwenye mechi hiyo ya fainali.
“Hakuwa na uhakika na hatima yake,” alisema Arteta alipozungumza na Daily Mail.
“Mara zote huwa anasema anataka kubaki lakini hajasaini mkataba, kwenye nusu fainali, hatukujua kitu gani kingetokea.
“Kama tungefungwa na Hull, habari
ingekuwa nyingine. “Ilikuwa mechi kubwa katika historia ya Arsenal,
tulishinda kombe la kwanza baada ya miaka tisa”.
Alex Oxlade-Chamberlain alionekana
katika mechi tano za Arsenal za Ligi Kuu msimu wa mwaka 2013-14, na
Arteta alisema mchezaji huyo wa kimataifa wa England alifanya makubwa
Emirates.
“Kiwango alicho nacho ni kikubwa, kama ataongeza jitihada, anaweza kufika mbali sana,” alisema Arteta.
“Ana kasi na uwezo wa kuwa winga bora, lakini ana mpango wa kuwa kiungo, na hilo ni gumu sana kulifanikisha".
Arteta pia alimzunguzmia kiungo Mesut
Ozil, aliyejiunga na klabu hiyo katika msimu wa ligi wa mwaka 2013-14
ambapo alionekana kumtetea.
Kiungo huyo wa Ujerumani aliigharimu
Arsenal pauni milioni 42.4 lakini mchezaji huyo wa zamani wa Everton
alisema bingwa huyo wa kombe la dunia ni msanii.
“Unapokuwa na mchezaji kama Ozil pamoja na mambo yote, watu wanaweza kumpenda ama kumchukia,” alisema Arteta.
“Unapokuwa msanii huwezi kucheza zaidi ya mechi 10 kila wiki, ni ngumu kwa mchezaji mbunifu kucheza hivyo”.
0 comments