
"Ripoti zinasema watu 20 wasio na hatia wamepoteza maisha", alisema Abdullahi Bego msemaji wa gavana wa Yobe Ibrahim Gaidam kuliambia shirika la habari la Anadolu.
Alisema wana mgambo hao wa Boko Haram waliwafyatulia risasi waislamu muda mfupi kabla ya kusaliwa sala ya Alfajiri.
"Hili ni janga. Serikali ina mamlaka ya kukomesha hili kundi licha ya jitihada zote bado wanaangamiza damu za wasio na hatia", alisema Abdullahi Bego.
Aliongeza kwa kutoa wito kwa wote walio nyuma ya mauaji haya waache kumwaga damu za wasio na hatia.
Zaidi ya watu 1,000 waliuawa katika miezi mitatu ya kwanza ya mwaka huu na kundi la Boko Haram.
0 comments